Ramin Mehmanparast amelaani oparesheni yoyote ya kigaidi katika
radiamali yake kwa madai yasiyo na msingi yaliyotolewa na viongozi wa
Marekani kwamba Iran imeshiriki katika mpango wa kutaka kutekeleza
oparesheni ya kigaidi huko Marekani. Ramin Mehmanparast amesema miamala
mibovu kama hiyo iliyojengeka juu ya siasa za kiadui na zilizopitwa na
wakati za Marekani na Uzayuni inatekelezwa kwa malengo maalumu na
maadui wa Uislamu na wa eneo hili. Ameongeza kuwa wapangaji wa njama
hizo hawana lengo jingine ghairi ya kuzusha hitilafu na kusaidia
kuuondoa utawala wa Kizayuni kwenye hali ya kutengwa.