Mwanzo    Nyumbani    Links   Kurasa ya kijani    Tafuta  



Brigedia Salami: Madai ya Marekani dhidi ya Iran ni hadaa
Namba: 271590 Tarehe: 1390/00/00Rejea: print

Marekani
Brigedia Salami: Madai ya Marekani dhidi ya Iran ni hadaa

Abna inatuarifu kuwa:Kamanda wa ngazi za juu wa Kikosi cha Kulinda Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran, Brigedia Hussein Salami amesema madai ya Marekani kwamba Iran ilihusika na njama ya kumuua balozi wa Saudi Arabia mjini Washington ni hadaa na hayaingii akilini. 

 Brigedia Salami: Madai ya Marekani dhidi ya Iran ni hadaa
Abna inaendelea kutuarifu kuwa:Brigedia
Salami amesema kuwa, madai hayo ya Marekani yasiyokuwa na mashiko wala
msingi ni moja  kati ya  njama za dola hilo la kibeberu za kujaribu
kuichanganya jamii ya kimataifa mkabala na kuelekea kufeli kwa mfumo
wake wa kibepari. Matamshi ya afisa huyo wa ngazi za juu wa jeshi la
Iran yanaenda sambamba na tamko la Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran
aliyesema kuwa, tuhuma hizo za Marekani ni mchezo uliofeli na hata
Wasaudia wenyewe wanaelewa vyema mchezo huo na taathira zake. Waziri wa
Mambo ya Nje wa Iran amesisitiza kuwa uhusiano wa Iran na nchi za Ghuba
ya Uajemi ni mzuri.Serikali Tehran imesisitiza kwamba, uhusiano wake na Serikali ya Riyadh ni mzuri licha ya hitilafu za kimtazamo ziliopo kati ya pande hizo
mbili kuhusu matukio ya eneo la Mashariki ya Kati.




 





 




Barua pepe:
Jina:
Ujumbe:
Enter security code
erfan
ABNA World Service
Englishالعربية
Françaisاردو
Españolفارسی
Русский中文
DeutschTürkçe
Azeri (cyr) Azeri (ltin)
Melayu Indonesia
বাংলা हिन्दी
Swahili Myanmar
BosanskiABP sites
  Habari za Zamani